Masaa ya kazi

Huduma za kuchukua alama za vidole                  Jumatatu hadi Ijumaa 10:00 Asubuhi – 12:30 Mchana

Uchukuaji wa pasipoti mpya                                     Jumatatu hadi Ijumaa 10:00 Asubuhi – 12:30 Mchana

                                                                                                                           02:00 Mchana – 03:30 Mchana

Maombi ya pasipoti yafanyika kwa “appointment”Ili kupanga tarehe ya kuja kuchukuliwa alama za vidole tafadhari bofya hapa.

A. Mahitaji:

  • Fomu ya pasipoti (CT 5) iliyojazwa kikamilifu kwenye vipengele vyote.
  • Picha tano (5) za pasipoti zenye “background” ya rangi ya “blue” au rangi ya maji ya bahari. (Ziwe za hivi karibuni).
  • Kivuli cha pasipoti ya zamani ukurasa 1 na ukurasa wenye picha na taarifa muhimu za muombaji (bio-data page).
  • Kivuli cha kibali cha makazi au Visa.
  • Kivuli cha cheti cha kuzaliwa/kiapo cha kuzaliwa cha mwombaji.
  • Kivuli cha cheti cha kuandikisha uraia wa Tanzania wa mwombaji.
  • Deed Poll ya badiliko la majina kwa wanaotaka kubadili jina.
  • Kivuli cha cheti cha ndoa kwa wanaotaka kubadilisha jina kwa sababu ya ndoa.

Kama pasipoti imepotea au kuibiwa ni lalzima kuleta:-

  • Loss report
  • Maelezo binafsi kwa maandishi kueleza yafuatayo:
  • Taarifa za pasipoti iliyopotea kwa maana ya Namba ya pasipoti, tarehe na mwaka ilipotolewa na DN yako;
  • Mazingira ya kupotea/kuibiwa kwa pasipoti; na
  • Mahali na tarehe ya kupotea/kuibiwa kwake.
  • Tangazo la gazeti kuhusu kupotea/kuibiwa kwa pasipoti hiyo.

Malipo ya maombi ya Pasipoti (Passport Application fees)

  1. Utaratibu wa Malipo:
  • Malipo ya Fomu ya Pasipoti:
  • Malipo ya fomu ya pasipoti ya £5.00 yanaweza kulipiwa kwenye kaunta yetu hapa Ubalozini kwa kutumiaKADI;
  • Kwa wale ambao hawawezi kufika Ubalozini malipo ya £5.00 yatafanywa kwa postal order ambapo mwombaji pia atatakiwa alete bahasha yenye anuani yake iliyobandikwa stempu za rejista ili apelekewe fomu; na
  • Kwa waombaji wanaoishi Ireland, malipo ya £5.00 ya fomu yatafanywa kwa Bank draft, ambapo pia atatakiwa alete bahasha yenye anuani yake pamoja na Bank draft ya £6.00 kwa ajili ya stempu ili apelekewe fomu hiyo (£5.00 ya fomu na £6.00 ya stempu zote pamoja zinaweza zikawa kwenye Bank draftmoja ya jumla ya £11.00).

 

Malipo ya Ada ya Pasipoti:

  • Kwa KADI kwa wale wanaofika kwenye kaunta zetu.
  • Kwa BANK TRANSFER – Barclays Bank

Sort Code: 20-71-74

Account No: 33205932

  • Kwa BANK DRAFT kwa wanaoishi Jamhuri ya Nchi ya Ireland.

Utaratibu wa Malipo (Payment methods)

Utaratibu wa Malipo:

  • Malipo ya Fomu ya Pasipoti:
  • Malipo ya fomu ya pasipoti ya £5.00 yanaweza kulipiwa kwenye kaunta yetu hapa Ubalozini kwa kutumiaKADI;
  • Kwa wale ambao hawawezi kufika Ubalozini malipo ya £5.00 yatafanywa kwa postal order ambapo mwombaji pia atatakiwa alete bahasha yenye anuani yake iliyobandikwa stempu za rejista ili apelekewe fomu; na
  • Kwa waombaji wanaoishi Ireland, malipo ya £5.00 ya fomu yatafanywa kwa Bank draft, ambapo pia atatakiwa alete bahasha yenye anuani yake pamoja na Bank draft ya £6.00 kwa ajili ya stempu ili apelekewe fomu hiyo (£500 hya fomu na £6.00 ya stempu zote pamoja zinaweza zikawa kwenye Bank draft moja ya jumla ya £11.00).

Malipo ya Ada ya Pasipoti:

  • Kwa KADI kwa wale wanaofika kwenye kaunta zetu.
  • Kwa POSTAL ORDER au BANK DRAFT kwa wanaoishi Ireland.
  • Kwa BANK TRANSFER.

Muda wa kushughulikia maombi ya Pasipoti:

Eligibility:

  • Pasipoti zinatolewa kwa Raia wa Tanzania tu. Hazitolewi kwa mwombaji ambaye anao urais wa nchi nyingine zaidi ya Tanzania.
  • Raia wa Tanzania ambaye amepata uraia wa nchi nyingine hana budi kurejesha pasipoti ya Tanzania Ubalozini kwa ajili ya kufutwa.
  • Pasipoti za Tanzania hazitolewi pia kwa watu wenye hadhi ya Ukimbizi.
  • Mtoto mwenye Uraia Pacha anaweza kupewa pasipoti ya Tanzania ikiwa hana pasipoti za nchi nyingine zaidi ya Tanzania.

NB: Waombaji wa pasipoti za Tanzania WANATAKIWA kusoma maelezo muhimu yanayohusu utoaji wa pasipoti kwenye FOMU Ukurasa wa 3 na 4.